· Jitambue (self awareness)
Tenga muda kila siku kujiangalia ndani yako
tambua mawazo yako hisia zako na namna unavyoitikia mambo.
Kuandika au kutafakarikimyakimya hukusaidia
kuanza safari ya kujijenga kwa uelewa.
· Jenga uhusiano wako wa Mungu/chanzo (Hatua ya kiroho)
Tenga muda wa sala kutafakariau shukurani
kila siku
Unganisha moyo wako na chanzo cha uhai.Roho
ikipata amani mabadiliko ya kweli huanza kuonekana kwenye Maisha yako.
SSOMA PIA:Unakunywa maji vizuri? fahamu faida unazokosa ukipuuza hii tabia.
· Jiweke malengo madogo na halisi
Usijisumbue na mipango mikubwa
isiyotekelezeka .anza na tabia ndogo kama kusoma kurasa chache ,kusali,kunywa
maji ya kutosha,au kunyoosha mwili. Hatua ndogo ndogo hujenga Imani ya ndani.
· Lisha akili yako kila siku
Chagua kile kinachoingia akilini mwako.
Soma maandiko ya kukuinua ,sikiliza mafunzo chanya au tazama vitu
vinavyokujenga kiakili na kimaadili.
· Jizungushe na mazingira chanya
Watu unaokaa nao na maudhuiunayoyafuata
vina nguvu kubwa.
Chagua mazingira yanayokutia moyo kukua siyo
yanayokurudisha nyuma.
· Jitunze kimwili
Mwili wako ni hekalu
Pata usingizi wa kutosha fanya mazoezi
mepesi na kula chakula chenye uhai.
Afya njema huisaidia akili na roho kukua.
SSOMA PIA:jinsi ya kutrack simu iliyoibiwa au kupotea na kuipata kwa haraka
KUMBUKA
Kujiboresha siyo kuwa mkamilifu,
Ni kuwa bora leo japo kwa uchache kuliko
ulivyokuwa jana.
Usisahau kukomenti,na kushare ili wengine
wajifunze.